- Get link
- X
- Other Apps
Top Stories
- Get link
- X
- Other Apps
Tanzania imeanza kwa ushindi katika mchezo wa Kundi B baada ya kuichapa Afrika Kusini mabao 2-1, katika mechi iliyomalizika hivi punde. Ushindi huo unaifanya Tanzania kuongoza Kundi B kwa muda ikiwa na pointi tatu.
Afrika Kusini ndiyo iliyotawala mchezo kwa kumiliki mpira kwa asilimia 64 dhidi ya asilimia 36 za Tanzania. Hata hivyo, Tanzania ilionyesha ufanisi mkubwa mbele ya lango kwa kutumia vizuri nafasi ilizozipata na kuondoka na ushindi muhimu.
Kwa mujibu wa takwimu za mchezo, Tanzania ilipiga mashuti nane, matano yakilenga lango, huku Afrika Kusini ikishindwa kutumia ubora wake wa kumiliki mpira kubadili matokeo ya mchezo.
Matokeo hayo yanaipa Tanzania mwanzo mzuri wa mashindano, huku ikiweka msingi imara kuelekea michezo ijayo ya Kundi B.

Comments
Post a Comment